Emmaus Shule ya Biblia
Emmaus Correspondence Bible School in DodomaEmmaus Shule ya Biblia inahudumia watu wote wanaopenda kusoma Biblia kwa njia ya posta. Masomo na mitihani yanatumwa kwa mwanafunzi. Baada ya kujaza anarudisha mtihani kwenye ofisi zetu.

Ilianzishwa kwa mara ya kwanza Tanzania mwaka 1960. Inafundisha Biblia kwa watu wa aina zote, na waumini wa dini zote. Haifundishi misingi wala mitazamo ya dhehebu lolote, bali ujumbe wa Neno la Mungu jinsi lilivyo.

Jina EMMAUS linatokana na jina la kijiji kimoja katika Biblia ambako wanafunzi wawili walikuwa wanaelekea walipotokewa na Bwana Yesu alipofufuka, Luka 24:13.

Kijiji hicho kiliitwa Emau kwa Kiswahili, na Emmaus kwa Kiingereza. („Emmaus“ ni tofauti kabisa na shirika la EMAU Tanzania ambalo ni kifupisho cha „Elimu ya Malezi ya Ujana“. Ili kuondoa utata, shule hii inatumia jina la Kiingereza, EMMAUS.)

Lengo la EMMAUS ni nini?

Wanafunzi wawili waliosafiri kwenda Emau (Emmaus), Bwana Yesu alipowatokea aliwafundisha mambo yaliyomhusu YEYE MWENYEWE; Luka 24:27. Hilo ndilo lengo kubwa la shule ya Emmaus: Kuwafundisha mambo yanayomhusu Mwokozi, na kuwaelekeza jinsi ya kukutana naye ili waweze kusema pia, „Je! mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, na kutufunulia maandiko?“ (Luka 24:32).

Mwanafunzi wa EMMAUS

Emmaus Correspondence Bible School in DodomaNi mtu gani anayeweza kujiunga kuwa mwanafunzi wa EMMAUS? Mtu yeyote anayejua kusoma na kuandika anakaribishwa kujifunza masomo ya EMMAUS. 


Sasa hivi EMMAUS ina wanafunzi 4,500 walio katika marika mbalimbali, kuanzia wanafunzi wa Shule za msingi mpaka watu wazima waliostaafu kazi. Wengine ni wakulima, wengine wafanya kazi wa nyumbani, wafanya biashara, waajiriwa maofisini, walimu, askari, n.k.





Masomo Ya Kiswahili

Somo / Ada
  • Kuchunguza Maandiko Matakatifu / bure
    Somo la kwanza - Download PDF (200KB)
    Mtihani - Download PDF (140KB)

  • Mungu Mmoja Njia Moja - 500/-
  • Mtumishi wa Mungu - 500/-
  • Mungu - 500/-
  • Neno la Mungu - 500/-
  • Njia ya Wokovu - 500/-
  • Chupa 12 za Maziwa - 500/-
  • Majuma Mawili ktk. Shule ya Maombi - 500/-
  • Maisha ya Mkristo - 500/-
  • Biblia Ifunzavyo - 500/-
  • Mwokozi wa Ulimwengu - 500/-
  • Mwenendo wa Mwamini - 500/-
  • Waraka kwa Warumi - 500/-
  • Je, Twaweza Kumjua Mungu - 500/-
  • Wanaume waliokutana na Bwana - 500/-

  • Petro na Kanisa - 800/-
  • Kukua Katika Imani - 800/-
  • Roho Mtakatifu na Kazi yake - 800/-
  • Biblia ni ya Ajabu - 800/-
  • Nyaraka za Yohana - 800/-
  • Safari katika Biblia - 800/-
  • Mambo Yajayo - 800/-

  • Chakula cha Bwana - 1000/-
  • 1 Wakorintho - 1000/-
  • Kuzikwa kwa Njia ya Ubatizo - 1000/-
  • Timotheo na Tito - 1000/-
  • Kristo Alilipenda Kanisa - 1000/-
  • Uvuvi wa Watu - 1000/-
  • Ufunuo - 1000/-
  • Al-Kitab - 1000/-
  • Matendo ya Mitume - 1000/-
  • Jifunze Biblia Nzima - 1000/-
  • Kitabu cha Mwanzo - 1000/-
  • Injili ya Marko - 1000/-


Maofisi wa EMMAUS

Emmaus Correspondence Bible School in DodomaEmmaus Shule ya Biblia
(Emmaus Correspondence Bible School)

P.O.Box 1424, Dodoma
Tanzania

Phone: +255 (0) 26 2350911
Email: This e-mail address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it
Location: Dodoma, Ipagala, Eneo la Emmaus,
off Dar Road

[ Pakua Ramani ]




Emmaus Correspondence Bible School in Dar es SalaamEmmaus Shule ya Biblia
(Emmaus Correspondence Bible School)

P.O.Box 9322, Dar es Salaam
Tanzania

Location: Dar es Salaam, Upanga, United Nations Road, Plot 358






Links

Shule za Emmaus katika nchi zingine:
[ http://www.emmaus.name ]

Shule za Emmaus katika nchi ya Kenya:
[ http://www.emmaus-kenya.info ]

Emmaus is a Correspondence Bible School operating in many countries. Check the international website for contacts in other countries [http://www.emmaus.name]. In Tanzania we have two offices serving the whole country.
 

Wasiliana nasi

Kanisa la Biblia Publishers
P.O.Box 1424, Dodoma
Tanzania

Phone: +255 (0) 26 2354 500
Mobile: +255 (0) 713 609166
Email: 
contact@klb-publishers.org

Location: Dodoma, Ipagala,
Eneo la Emmaus, off Dar Road

Washiriki wetu